Image
Image

Kenyatta asema kamwe hatakabidhi raia wake wa Kenya kwa ICC.


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema kamwe hataruhusu raia wake kukabidhiwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ICC kutokana na vurugu zilizotokea kwenye uchaguzi wa mwaka 2007- 2008, zilizosababisha vifo vya watu 1,200 na wengine laki 6 kupoteza makazi yao.
Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Nakuru, Rais Kenyatta amesema ushirikiano wa miaka mitano kati ya Kenya na ICC umekwisha, na sasa Kenya itatatua matatizo yake kwa kutumia mahakama zake. Mkutano huo ulihudhiriwa na naibu rais Bw William Ruto, mwanahabari Joshua Sang, na maofisa wengine ambao ICC ilifuta kesi zao.
Kauli ya Rais Kenyatta imekuja wakati ICC imetoa hati ya kuwaita mahakamani raia wengine watatu wa Kenya kujibu tuhuma za kuingilia kesi ya Bw Ruto na Bw Sang.
Ingawa Kenya inabanwa kisheria kushirikiana na ICC, wabunge wa nchi hiyo wametishia kuiondoa Kenya kwenye mahakama hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment