Image
Image

Madereva wa daladala wagoma kutokana na ubovu wa barabara Songea.


Madereva wa Daladala zinazofanya safari zake kutoka Mjini kati naMkuzo,Mwengemshindo  Mjini Songea wamegoma  kwa siku  moja  kutokana na ubovu wa  barabara  na kuamua kutengeneza barabara ya Mkuzo-Mauki ambayo ni  mbovu na hivyo wameiomba serikali kuitengeneza barabara hiyo.
Wakitengeneza barabara hiyo  kwa kushirikiana na makondakta wao pamoja na  madereva wa bodaboada wamesema kuwa wameamua kusitisha usafiri wa daladala kwa muda  kutokana na ubovu wa barabara unaosababisha magari yao kuharibika na hivyo wameamua kuitengeneza wao wenyewe.
Kwa upande wao wananchi wamezungumzua wakati mgumu waliokutana nao kutokana  na ubovu  huyo wa barabara.
Kwa upande wake  mhandisi  wa  barabara wa manispaa ya songea  Godfrey Majuto   anasema kuwa  wametenga shilingi milioni  kumi na sita kurekebisha  barabara hiyo itakapopungua mvua wakati wakisubiri bajeti ya mwaka 2016/2017 na kwamba  hakuna mpango wa kuitengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha lami  kwa sasa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment