Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanaia Dr.John
Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa mkoa wa shinyanga Ana kilango Malecela
kuanzia leo
Utenguzi huo umetokana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo
Ana kilango Malecela kutungaza kwenye vyombo vya habari kuwa mkoa wake hauna
watumishi hewa jambo ambalo lilisababisha Ikulu kufanya uchunguzi wake na
kubaini kuwepo kwa wafanyakazi hewa 45 katika awamu ya kwanza na awamu ya pili
ya uchunguzi bado inaendelea.
Akiongea Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akipokea
hundi ya shilingi bilioni sita zilizotolewa na Ofisi ya Bunge baada ya kubana
matumizi kwa ajili ya kununulia madawati Rais Magufuli ameeleza kusikitishwa na
hali hiyo na kuagiza Mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa kuondolewa ofisini
mara moja.
0 comments:
Post a Comment