Image
Image

Panama:Aliyekuwa rais wa Argentina taabani


Kiongozi wa mashtaka nchini Argentina ameomba idhini ya mahakama kuanzisha uchunguzi katika shughuli za aliyekuwa rais wa taifa hilo, Cristina Fernandes de Kirchner, juu ya madai kuwa alishiriki katika utakasaji wa pesa haramu.
Uamuzi huo unafuatia ushahidi uliotolewa mahakama Ijumaa na mfanya biashara, Leonardo Farina mshirika wake yeye na mumewe ambaye pia alikuwa ni rais wa Argentina bwanaNestor Kirchner .
Akitoa ushahidi baada ya kuahidiwa kusamehewa makosa yake mfanyabiashara huyo alisema kuwa Bi Fernandez na marehemu mumewe Nestor Kirchner walishiriki katika shughuli kadhaa ya ulaghai wa fedha za umma.
Mfanyabiashara mwingine ambaye pia ni mwandani wa familia ya Kirchner, Lazare Baez, alitiwa mbaroni mapema juma lililopita na kulaumiwa kwa ulaghai wa Dola Milioni tano.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment