Image
Image

Polisi lamnasa Mwanamume aliyetumia silaha kwa unyang’anyi na kukimbia Morogoro.



Na.Devotha Songorwa,Morogoro.
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia Mwanamume Mmoja aitwaye SATOTI MAHENGE kwa kosa la Unyang’anyi kwa kutumia Silaha katika kijiji cha Dodoma Tarafa ya Mlali wilayani Mvomero Mkoani Morogoro.
Mtuhumiwa huyo umri (33) ambaye ni mkazi wa Mafinga Mkoani iringa pamoja na wenzake watano ambao hawajafahamika mara moja    walitega gogo katika barabara kuu ya Iringa Morogoro na kusimamisha gari lenye namba za usajili T,372 DCL MITSUBISHI CANTER na kufanikiwa kupora simu 5 na fedha Taslimu 310000 na kisha kuwajeruhi  watu 4 ambao walikuwa ndani gari hilo ambapo mpaka sasa wamefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja.
Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro URICH MATEI amebainisha hayo Mbele ya waandishi wa habari na kusema kuwa mtuhumiwa huyo wanamshikilia zaidi kwa uchunguzi kusudi pia kuweza kupata jopo zima la watu aliokuwa akishirikiana nao.
Kwa upande mwingine pia kamanda MATEI ameongeza kuwa wanamshikilia mtuhumiwa mmoja anayefahamika kwa jina la BERNARD AMON,miaka 30, mkazi wa Mawezi mlinzi wa kampuni ya QUICK SECURITY ambapo anatuhumiwa kwa kufyatua risasi kwa uzembe na kusababisha majeraha kwa watu 2 ambao ni RAMADHANI JAMES Miaka 21,mkazi wa Nanenane Oilcom na HUSSEIN ALLY,miaka 27 ,mkazi wa kilakala ambaye alijeruhiwa mguu wa kushoto.
Hatahivyo kamanda MATEI amesema kuwa watuhumiwa wote wapo mikononi mwa polisi na wanaendelea kuhojiwa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment