Image
Image

Hali ni mbaya kwa wananchi wa Chanika kwa kunywa maji ya vinyesi vya binadamu Tanzania.


Licha ya Serikali kupaza sauti juu ya wananchi kuwa na tabia yakuwa wasafi sehemu wanazo ishi lakini hali bado inaonekana kujitokeza kuwa tofauti ambapobaadhi ya wakazi wa wilaya ya Handeni hatarini Mkoani Tanga Afya zao zipo hatarini baada ya kunywa maji yanayotokana na vinyesi vya binadamu.
Inaelezwa kuwa hadi kufikia hatua hiyo ni kutokana na wananchi wa kukaidi maagizo ya kuchimba vyoo na hivyo kujisaidia Pembezoni mwa Bwawa lililopo mji wa Chanika Wilayani humo lenye maji yanayotumiwa na sehemu kubwa ya wakazi wake kisha vinyesi vyake hutiririka wakati mvua ikinyesha na wananchi kuchota na kuyatumia bila kuchemsha.
Mganga mkuu wa wilaya ya Handeni Dr,CrediaNus Mgimba amesikitishwa na kitendo cha wakazi hao kutumia maji ya vinyesi na kuwataka kuacha mara moja kutumia maji hayo yenye vinyesi na wasio yachemsha na kuwataka wakulima wanaolima pembeni mwa bwawa hilo nao kuacha kutumia eneo hilo kujisaidia ili kudhibiti milipuko ya ugonjwa ya kipindupindu.
Wakazi wa eneo hilo wamekiri wazi kuwa maji hayo si salama kiafya na hivyo kuiomba serikali kuweza kuwaboreshea miundo msingi kwenye bwawa hilo ili kuzuia mtiririko wa vinyesi vinavyokwenda katika maji ili kunusuru afya zao.
Kwaupande wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Husna Msangi amewataka wananchi kuzingatia kanuni za afya ili kuepukana na  magonjwa ya milipuko ikiwa ni pamoja na kuchimba vyoo,kuchemsha maji ya kunywa,kunawa mikono na sabuni.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment