Image
Image

Mlipuko wa homa ya manjano umewaua watu 21 DRC Kongo.


Mlipuko wa homa ya manjano umewaua watu 21 katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani{WHO}, homa hii imetoka katika nchi jirani ya Angola.
Taarifa ya WHO inasema vifo hivyo vilitokea mwezi Machi huku kukiwa na visa vingine 151. Kuna hofu huenda mulipuko huu ukasambaa zaidi. Homa hii ya manjano imewaua watu 225 nchini Angola na kuwaambukiza wengine 1,600.
WHO imeongeza kwamba maafisa wa DRC wameweka vituo vya dharura kushughilikia mulipuko huo.Aidha raia wanaosafiri nchini Angola watapewa chanjo dhidi ya ugonjwa huo. Homa hii husababisha kuvuja damu na figo kushindwa kufanya kazi.
Inaambukizwa na aina ya mbu {Aedes aegypti}. Maeneo yaliyo kwenye hatari ya Homa ya manjano ni pamoja na Bara Afrika na Amerika Kusini.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment