Image
Image

Polisi wa Chicago nchini Marekani waelezwa kuwa wabnaguzi wa rangi.



Polisi katika mji wa Chicago nchini Marekani wamejawa na ubaguzi wa rangi, imesema ripoti mpya rasmi.
Ripoti hiyo imetayarishwa na jopo maalum lililoundwa kutokana na ghadhabu ya umma baada ya polisi kulaumiwa kwa kuwapiga risasi kiholela raia wasio Wazungu.
Jopo hilo limesema polisi waliwalenga watu weusi na jamii ya Latino na hutumia nguvu kupita kiasi kukabiliana nao.
Ripoti hii imependekeza mageuzi 100.
Asilimia 74 ya mamia ya watu waliouawa na maafisa wa polisi walikuwa raia weusi, licha ya kwamba idadi ya watu weusi ni asilimia 33 pekee.
Idara ya polisi mjini Chicago ndiyo ya tatu kwa ukubwa nchini Marekani.
Aidha visa vya mauaji katika mji huo vilipanda kwa asilimia 84 mwaka huu ikilinganishwa na mwaka uliopita.
Kulizuka maandamano ya umma pale afisa wa polisi Mzungu alipompiga risasi na kumuua kijana mweusi.
Maandamano hayo yalichochea Wizara ya Haki ya Marekani kuanzisha uchunguzi dhidi ya mauaji hayo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment