Image
Image

Taarifa zakwamba Makamu wa Rais ameagiza kuzimwa data za simu saa zakazi Zakanushwa.




Ikiwa imepita siku moja tu kwa mitandao ya kijamii kuonekana ikisambaa taarifa inayodai kwamba Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameyataka makampuni ya simu za mkononi kuzima data zao kila siku kuanzia saa 2.30 asubuhi mpaka saa 10.30 jioni ili kuzuia Watanzania kuwa online kipindi cha muda wa kazi na masomo kwa wanafunzi taarifa hizo zakanushwa.
Taarifa hizo zimekanushwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na kusema kuwa Makamu wa Rais hahusiki na wala hajawahi kutoa agizo hilo hivyo Ofisi hiyo inawataka watanzania kuwa makini na taarifa ambazo zinaibuliwa tu na watu wasio julikana wakiwa na sababu zao kuzipuuza kwani taarifa hizo ni za uzushi.
Hata hivyo Ofisi hiyo ya Makamu wa Rais imetoa onyo kali kwa watu wanaosambaza taarifa hizo za uzushi na kuwataka watanzania kuwafichua watu wa namna hiyo wenye tabia ya kutoa taarifa za uongo kwa kutumia jina la kiongozi huyo.
Pia Mheshimiwa Makamu wa Rais amewasihi watanzania kutumia muda mwingi kuchapa kazi ili kujipatia maendeleo kwenye maisha yao na siyo kutumia muda mwingi kufanya shughuli ambazo siyo za maendeleo kwa maisha yao binafsi.
Aidha Serikali na vyombo vya usalama inaendelea kuwasaka watu wanaochafua majina ya viongozi wakubwa wa nchi na watu wengine kwa taarifa za uzushi na kuwachukulia hatua kali za Kisheria ikiwemo ile ya Makosa ya Mtandao..
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment