Image
Image

Watu tisa wafa zaidi ya 700 wajeruhiwa baada ya kutokea tetemeko la ardhi Japan


Watu tisa wamekufa  na wengine  zaidi ya mia saba wamejeruhiwa baada ya kutokea tetemeko la ardhi katika kisiwa cha kyushu kilichopo  kusini mwa nchi ya japan.
Maafisa wamesema watu zaidi huenda bado wamenaswa kwenye vifusi vya majengo yaliyoanguka huku maelfu wakikimbia makazi yao na watu wengi wamekesha pembezoni mwa mji wa mashariki  kwenye kisiwa hicho cha kyushu.
Waziri mkuu wa japan shinzo abe amesema kwa serikali imetuma polisi, wazima moto na wanajeshi kuendesha operesheni za uokoaji na kuwataka waliokumbwa na tukio hilo kuwa na subira wakati jitihada za serikali za kuwaokoa zikiendelea.
Mpaka sasa hospitali nchini japan bado zinawapokea waathirika wa tetemeko hilo kubwa la ardhi  lililokuwa na  kipimo cha richter  6.3  ambalo liliambatana na mengine madogo kadhaa.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa matetemeko hayo madogo yanaendelea licha ya kwamba baadhi  ya watu wameamua kurejea hivyo hivyo katika makazi yao kwa kuyaona hayatakuwa na madhara kwao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment