Image
Image

Nigeria yaonesha wasiwasi wake juu ya video ya wasichana waliotekwa na Boko Haram.


Nigeria imeelezea wasi wasi wake na mashaka ya mkanda mpya wa video wa kikundi cha boko haram unaoonyesha picha za baadhi ya wasichana wanaodaiwa kuwa wa shule ya chibok.
Mkanda huo unaonyesha picha za wasichana 15 waliovaa mavazi meusi na bluu nyepesi wanaodaiwa kuwa ni miongoni mwa wasichana 276 waliotekwa miaka miwili iliyopita kwenye shule ya sekonari ya chibok.
Waziri wa habari wa nigeria bwana lai mohamed amesema mpaka sasa serikali ya nchi  yake haina uhakika kwa asilimia mia moja kama wasichana hao ndiyo wale waliotekwa au la.
Pia makundi ya watu ambao wamepotelewa na ndugu zao wamekuwa wakikusanyika katika makundi makundi na kuanza kuziangalia sura zinazoonekana kama ni za ndugu zao au la.
Katika maeneo mengine nchini humo  maandamano yameendelea kufanyika kuishinikiza serikali ya nchi hiyo kuongeza jitihada za kuwatafuta na kuwaokoa wasichana hao ambapo hawajulikani walipo hadi sasa.
Kikundi cha kiislamu cha boko haramu kiliwateka wasichana zaidi ya mia mbili miaka miwili iliyopita wakiwa shuleni na kutokomea nao kusikojulikana ikiwa ni hatua ya kuishinikiza serikali ya nigeria kutekeleza matakwa yao.
Matakwa hayo ni kutumika kwa sheria za kiislamu katika baadhi ya maeneo ya kaskazini mwa nchi hiyo hasa katika mji wa maiduguri kitu kilichopingwa na serikali na baadaye wakaanzisha harakati za kijeshi dhidi ya serikali.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment