Image
Image

Zaidi ya watu 100 wafa 200 wajeruhiwa kwa moto uliozuka kwenye hekalu la wahindu nchini india.



Watu zaidi ya 100 wamekufa na wengine zaidi ya 200 wamejeruhiwa kutokana na moto uliozuka kwenye hekalu la wahindu nchini india.
Wengi wa waliojeruhiwa hali zao ni mbaya na wanatibiwa  kwenye hospitali ya chuo kikuu katika mji wa Thiruvananthapuram,ambao ni mji mkuu wa jimbo la Kerala.
Moto huo umezuka leo alfajiri  na umenzia kwenye fataki zilizokuwa zimehifadhiwa kwenye hekalu hilo linaloitwa Puttingal,kwenye mji wa pwani wa Paravur  katika jimbo la Kerala .
Fataki hizo hizo zilikuwa zitumike kwenye sherehe za mwaka mpya wa wahindu.
Maelfu ya watu walikuwemo kwenye hekalu hilo,wakati mlipuko mkubwa uliposikika majira ya alfajiri na  moto kuenea kwenye jengo hilo na watu wengi kunaswa ndani.
Waziri mkuu wa india,  narendra modi  amekwenda kwenye eneo la tukio kujionea hali halisi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment