Hillary Clinton amepata ushindi muhimu katika kura ya mchujo jana katika mji mkuu wa Marekani, ikiwa ni kura ya mwisho katika kura za mchujo kuelekea uchaguzi wa rais kwa mwaka huu 2016, wakati hali sasa inahamia katika mpambano dhidi ya hasimu wake kutoka chama cha Reupblican Donald Trump.
Clinton alishinda kwa asilimia 79 dhidi ya asilimia 21 alizopata Bernie Sanders, wakati ambapo kura karibu zote zimekwisha hesabiwa.
Huu ni mwisho mbaya kwa seneta Bernie Sanders wa jimbo la Vermont, ambaye alileta hamasa nyingi kwa Waliberali na wapiga kura huru kwa kampeni katika matawi ambayo ilileta changamoto kubwa dhidi ya Clinton.
Clinton na Trump wameshaanza kutupiana maneno na kutoa misimamo tofauti katika kupambana na ugaidi kufuatia mauaji katika klabu ya mashoga mjini Orlando.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment