Mawaziri wa kilimo wa kundi la nchi 20 G20 wameahidi kuunga mkono uvumbuzi na maendeleo endelevu ya kilimo.
Ahadi hiyo imetolewa kwenye mkutano wa mawaziri hao u7liofanyika mjini Xi'an, China. Mkurugenzi wa taasisi ya sera ya chakula ya kimataifa Bw. Fan Shenggen amesema mkutano huo umeweka msisitizo katika usalama wa chakula, kufanya uvumbuzi wa teknolojia ya kilimo na kuzitumia pamoja teknolojia hizo.
"Kwanza, kundi la G20 linatilia maanani katika usalama wa nafaka, kilimo na chakula. Pili, linasisitiza uvumbuzi. China siku zote inahimiza uvumbuzi wa teknolojia, sera na mfumo. Tatu, taarifa ya mkutano imeweka bayana hatua za utekelezaji, ambazo ni pamoja na jinsi nchi wanachama zinavyonufaishana na kubadilishana ujuzi. Mbali na hayo, jambo lingine ni kujenga jukwaa la uvumbuzi kupitia mtandao wa Internet, ambao unaunganisha familia, masoko na teknolojia."
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment