Mkutano wa 169 wa Jumuiya ya nchi zinazozalisha mafuta OPEC umeshindwa kufikia makubaliano kuhusu kikomo cha uzalishaji wa mafuta ghafi.
Hii ni mara ya pili kwa nchi za OPEC kushindwa kufikia makubaliano kuhusu kikomo kipya cha juu cha uzalishaji wa mafuta tangu mkutano wa mwishoni mwa mwaka jana.
Hivi sasa uzalishaji wa mafuta wa jumuiya hiyo uko katika kiwango cha pipa milioni 32 kwa siku.
Bei ya mafuta ya kimataifa imekuwa ikishuka, na ilishuka hadi kufikia dola 26.21 za kimarekani kwa pipa mwezi Februari, ambayo ni bei ya chini zaidi katika miaka 12 iliyopita, lakini kuanzia mwanzoni mwa mwezi wa Machi, bei hiyo imeanza kuongezeka.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment