Image
Image

KIJAJU:Sheria ya kukusanya kodi ya magari inayoitwa Motor IMEANZA.

Bunge limeambiwa kuwa  Serikali  imeanza mchakato wa  kuboresha sheria ya kukusanya kodi ya  magari  inayoitwa Motor Vihicle au Road  Licence  ikiwa ni pamoja na  kutoa mapendekezo  ya namna bora ya  kuhudumia  wamiliki  wa magari  ambayo  yatakuwa  yamesimama  kwa kipindi  kirefu bila ya kutembea  barabarani  kwa sababu za  msingi.
Hayo   yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango,Dakta    ASHATU  KIJAJU  alipokuwa   akijibu swali la  Mbunge wa Nkasi Kusini,   DESDERIUS  MIPATA  aliyetaka  kujua Serikali  inampango  gani wa kuitizama upy a sheria hiyo .
Dakta  KIJAJU  amesema kuwa  sheria hiyo haitoi unafuu wowote kwa gari lililosimama kwa  muda mrefu  bila  ya kutembea  barabarani  akaongeza kuwa  utaratibu huo   umekuwa unaleta adha kwa wamiliki wa  magari na hasa pale ambapo kuna usha h idi  wa kutosha kwamba  gari husika limesimama kwa muda  mrefu kwa sababu  za msingi.
Akaongeza kuwa  baada ya  taratibu  zote  kukamilika  mapendekezo  ya  mabadiliko  ya sheria  hiyo  itapelekwa  bungeni ili kujadiliwa  na k uiidhinishwa  na bunge  kwa kad iri  itakavyoonekana  inafaa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment