Image
Image

Obama ashutumu matamshi ya Donald Trump dhidi ya mauaji ya wapenzi wa jinsia moja.

Rais  wa  Marekani Barack Obama  ameshutumu  matamshi ya  Donald Trump  kufuatia  mashambulizi  ya  kinyama  ya risasi ambapo  watu  49  waliuwawa  katika  klabu  ya mashoga jimboni  Florida mwishoni  mwa  juma.
Trump ambaye anaelekea  kupata  uteuzi  kuwa  mgombea wa  urais kwa tiketi  ya  chama cha  Republican, alitumia mashambulizi hayo  kuongeza  kasi  katika  matamshi  yake dhidi  ya  Uislamu, akirudia  miito  yake  ya  kutaka kupigwa  marufuku  kwa  muda  Waislamu  kuingia  nchini Marekani.
Katika  hotuba, Obama  alimweleza Trump  kuwa  ni kitisho kwa  usalama  wa  taifa.
Matamshi  ya  rais  Obama  yanafuatia ukosoaji  ulitolewa na  Trump  dhidi  yake , ambae  alisema  Obama analazimika  kujiuzulu  kwasababu  amekataa  kuyaeleza mashambulio  ya  Orlando  kuwa  ni tukio la Uislamu wa itikadi  kali.
Wakati  huo  huo  mke wa  mshambuliaji  huyo  wa Orlando, Omar Mateen, anaweza  kushitakiwa  kuwa ni mshirika  wa  shambulio  hilo, kwasababu  huenda alifahamu  kwamba  mume  wake  anapanga mashambulizi.
Jopo  la  washauri  wa  mahakama  limeundwa  na linaweza  kuanza  kazi  kuanzia  mapema  leo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment