Serikali imesema inafanya jitihada kuziwezesha hospitali za Rufaa za mikoa zinatoa huduma za matibabu ya Fistula.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , UMMY MWALIMU alipokuwa kijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,MGENI JADI KADIG A aliyetaka kuju a serikali ina mapango gani wa kutokomeza tatizo la ugonjwa wa Fistula nchini.
Ameliambia bunge kuwa tatizo la fistula linatokana na mjamzito kupata uchungu pingamizi kwa muda mrefu na kwamba tatizo hilo linaweza kuepukwa kwa kuboresha huduma kwa wajawazito .
Amesema ili kuboresha huduma kwa wajawazito wizara imekuwa inatekeleza hatua mbalimbali kama kuelimisha jamii kupitia huduma za afya katika jamii na vyombo vya habari kuhusu umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma ya afya.
Like ukurasa wetu wa Facebook hapo, kwa kuweza kupata taarifa zaidi, kila zinapo tufikia.
Home
News
Slider
Serikali kuziwezesha Hospitali za rufaa za mikoa zinatoa huduma ya Matibabu ya Fistula.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment