David
Cameron ameongoza kikao chake cha mwisho cha baraza la mawaziri baada
ya kuwa waziri mkuu wa Uingereza kwa miaka sita ambapo anampisha katika
nafasi hiyo waziri wa mambo ya ndani Theresa May kujiandaa kuunda
serikali mpya baada ya kura ya kujitoa katika Umoja wa Ulaya.
Kuondoka
madarakani kwa Cameron kumekuja mapema kuliko ilivyotarajiwa kufuatia
mabadiliko ya ghafla katika kinyang'anyiro cha kumrithi ambapo naibu
waziri wa nishati Andrea Leadsom alijitoa dakika za mwisho na kumuachia
Theresa May kuibuka mshindi wa wazi katika chama hicho cha
Conservative. Leo
waziri mkuu David Cameron atawasilisha barua yake ya kujiuzulu kwa
Malkia Elizabeth wa pili na kutoa nafasi kwa Theresa May kuanza mara
moja majukumu yake kama waziri mkuu mpya ikiwa ni pamoja na kuunda
serikali.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment