India imeipatia Tanzania dola za Kimarekani milioni 500 kwa ajili ya miradi ya maendeleo ili kukuza ushirikiano wa kiuchumi baina nchi hizi mbili.
Hayo yamesemwa jijini Dar es
Salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John
Pombe Magufuli katika dhifa ya kitaifa aliyomwandalia mgeni wake,
Waziri Mkuu wa India, Mheshimiwa Narendra Modi.
“Tunaishukuru India
ambayo imeonyesha utayari wa kushirikiana nasi kiuchumi katika kilimo,
TEHAMA, maji, Elimu, Afya na Ulinzi,” amesema Rais Magufuli.Rais
Magufuli pia amesema ushirikiano wetu na India utatoa fursa kwa Tanzania kutimiza azma yake
ya kuwa na uchumi wa viwanda kwani katika ziara hii Waziri Mkuu
ameambatana na wafanyabiashara takriban 50 ambao wanaangalia fursa za
kibiashara hapa nchini.
Home
News
Slider
India imeipatia Tanzania dola za Kimarekani milioni 500 kwa ajili ya miradi ya maendeleo
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment