Image
Image

JWTZ laungana na majeshi ya mataifa mengine 4 kukabiliana na Ugaidi.

Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limeungana na majeshi ya mataifa mengine manane kufanya mazoezi ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao ukiwamo ugaidi, dawa za kulevya na uharamia.
Akifungua mafunzo hayo Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi ameeleza kuwa kutokana na mabadiliko ya vyanzo vya migogoro katika jamii ya kimataifa, majeshi ya ulinzi nayo hayana budi kuwaendeleza askari wake uwezo wa kukabiliana nayo ili kudumisha amani.
“Zamani tulikuwa tunajipanga kulinda mipaka yetu na kufanya maandalizi ya vita na yeyote atakayetushambulia. 
Hali imebadilika sasa hivi. Uharamia, ugaidi na dawa za kulevya ndiyo tishio la usalama kwa nchi nyingi duniani,” amesema waziri huyo.
Amesema kutokana na makosa hayo kutekelezwa kwa mitandao mikubwa duniani yanahitaji ushirikiano baina ya wadau mbalimbali ndani ya jamii ambao wataunganisha nguvu, ujuzi na uzoefu ili kupunguza kama si kutokomeza kabisa athari zake.
Dk Mwinyi amesema juhudi za Serikali nyingi duniani kukabiliana na uhamishaji wa binadamu pamoja na uharamia umesababisha hasara kubwa ambazo zinahitaji mikakati imara itakayohakikisha biashara na maisha kwa ujumla yanastawi pasipo kikwazo chochote kutoka kwa watu wachache.
Amesema hayo mbele ya maofisa wa Shirika la Msalaba Mwekundu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) na Umoja wa Afrika (AU).


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment