Image
Image

Erdogan kukutana na Putin.

Katika  ziara  yake  ya  kwanza  nje  ya  nchi  tangu kushindwa  kwa  jaribio  la  mapinduzi mwezi  uliopita, Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki anatarajiwa  kukutana na  Rais Vladimir Putin mjini  St. Petersburg leo.
Hapo jana, Erdogan alisema ziara hiyo ni alama mpya katika uhusiano kati ya nchi  hizo mbili.
Rais huyo  wa  Uturuki  amesema  anataka kuanza  tena upya  uhusiano  wa  kijeshi, kiuchumi  na  kiutamaduni.
Uhusiano  wa  Uturuki  na  mataifa  ya  Ulaya  na  Marekani umeathirika  wakati  serikali mjini Ankara ikifanya  msako dhidi  ya  maelfu  ya  wanaodaiwa  kuwa  waungaji  mkono wa  jaribio  hilo  la  mapinduzi  lililoshindwa.
Uhusiano  na  Urusi  ulichafuka  baada  ya  Uturuki kuiangusha  ndege  ya  kijeshi  ya  Urusi  karibu  na mpaka  na  Syria mwezi Novemba  mwaka  jana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment