Kikosi maalumu cha jeshi la Ufaransa huenda kumejiunga na katika kambi ya jeshi ya Marekani inayopatikana Malte.
Taarifa hiyo imetolewa na vuanzo vya habari vya asalama nchini Libya.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa ni kwamba kikosi maalumu kutoka Ufaransa kilichokuwa kikimuunga mkono jenerali Khalifa Haftar kimeondoka Benghazi mashariki mwa Libya.
Kikosi hicho kimeripotiwa kuondaka katika eneo hilo siku tatu zilizopita.
Vyanzo vya habari vimefahamisha kuwa kikosi hicho kimerejea katika kambi yake ya zamani.
Taarifa zaidi zinafahamisha kuwa katika siku za nyuma kumeonekana kupungua kwa kiasi kikubwa kwa ndege za jeshi angani.
Hakuna taarifa yeyote ambayo ilitolewa ikielezea sababu za jeshi la Ufaransa kuchukuwa aumuzi wa kuondoka Benghazi.


0 comments:
Post a Comment