Image
Image

Urusi na Uturuki yathibitisha kuwa na malengo sawa kuhusu Syria.

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki  Mevlut Cavusoglu afahamisha kuwa Uturuki na Urusi ipo katika mstari mmoja kuhusiana na suluhisho la kisiasa la mzozo wa Syria pamoja na msaada kwa raia wa Syria.
Cavusoglu katika maelezo yake alisema kuwa serikali zote mbili za Uturuki na Urusi hazingependa kuona kuendelea kwa mauaji ya raia wasio na hatia Syria,na pia hawaoni sawa Aleppo kukabiliwa na mashambulizi mara kwa mara .
Aidha Cavusoglu alifahamisha kuwa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi hizo mbili pamoja na jeshi wakishirikiana na idara ya upelelezi watashirikiana katika shughuli za usalama .
Cavusoglu alisema pia watafanya ushirikiano na Urusi katika sekta ya Ulinzi hasa ikiwa pia Uturuki ni mojawapo ya nchi ambazo ni mwanachama wa NATO.
Kuhusu suala la kuangushwa kwa ndege ya kivita ya Urusi mnamo Novemba 24 mwaka jana,waziri huyo alifahamisha kuwa wahusika wa kitendo hicho tayari wamekamatwa na wanaendelea kuulizwa maswali kuhusiana na suala hilo.
Alisema kuwa hiyo ilikuwa mojawapo ya mipango ya kundi l FETO katika juhudi za kuharibu uhusiano baina ya Uturuki na Urusi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment