Mwanasoka
shujaa wa Brazil katika mchezo wa soka katika michuano ya Olimpiki,
Neymar ameonekana akishangilia timu ya mpira wa wavu ya wanaume ya
Brazil katika mchezo wa fainali ambao walishinda medali ya dhahabu.
Neymar,
ambaye amejivua wadhifa wa Kapteni wa Brazil, alifunga penati ya
ushindi dhidi ya Ujerumani na kusaidia Brazil kutwaa medali ya dhahabu
pamoja na kulipa kisasi cha kufungwa na Ujerumani katika mchezo wa nusu
fainali za kombe la dunia.
Timu
ya mpira wa wavu ya Brazil iliishinda Italia jana na kutwaa medali ya
dhahabu na kuchangia kuweka rekodi bora ya Brazil katika michuano hiyo
kwa kutwaa medali saba za dhahabu katika michuano hiyo ya Rio 2016.
Wachezaji wa mpira wa wavu wa Brazil wakishangilia ushindi.



0 comments:
Post a Comment