Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru
Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna
Mufaddal Saifuddin mara baada ya kuchangia madawati kwa kutoa hundi
yenye thamni ya kiasi cha dola za Kimarekani (USD 53,000) kwa ajili ya
utengeezwaji wa madawati.............................................................................................................................
Kiongozi
Mkuu wa Jumuiya ya DAWOODI BOHRA duniani Mtukufu Dakta SYEDNA MUFADDAL
SAIFUDDIN SAHEB amemkabidhi Rais JOHN MAGUFULI hundi.
Kiongozi Mkuu
wa Jumuiya ya DAWOODI BOHRA duniani Mtukufu Dakta SYEDNA MUFADDAL
SAIFUDDIN SAHEB amemkabidhi Rais JOHN MAGUFULI hundi ya Dola Elfu 53 za
Kimarekani ambazo ni sawa na Shilingi Milioni 116 za Kitanzania kwa
ajili ya kuchangia utengenezaji wa madawati ya wanafunzi kwa shule
mbalimbali hapa nchini.
Dakta SAIFUDDIN SAHEB amekabidhi hundi hiyo
Ikulu Jijini DSM alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais MAGUFULI
ambapo pia amekabidhi hundi nyingine ya Dola Elfu 23 za Kimarekani
ambazo ni sawa na Shilingi Milioni 46 kwa ajili ya Baraza Kuu la
Waislamu Tanzania - BAKWATA.
Mazungumzo haya yamehudhuriwa pia na
Mufti wa TANZANIA Sheikh ABOUBAKAR ZUBEIR na Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dakta AUGUSTINE MAHIGA ambapo Rais
MAGUFULI amewakaribisha wana Jumuiya hiyo kuwekeza hapa nchini.
Rais
MAGUFULI pia amewakaribisha Wanajumuiya hao katika Maadhimisho ya
Jumuiya ya DAWOODI BOHRA duniani yanayotarajiwa kufanyika Jijini DSM
Mwezi Oktoba mwaka huu.
Katika hatua nyingine, Rais MAGUFULI amepokea
barua kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya SAHARAWI, -BRAHIM GHALI
iliyowasilishwa na Mjumbe Maalum wa Rais huyo ambaye ni Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais BACHIR MOUSTAPHA SAYED.
Pamoja na kupokea barua hiyo
Rais MAGUFULI amesema Serikali yake itaendeleza na kuimarisha zaidi
ushirikiano wake na Jamhuri ya Kiarabu ya SAHARAWI na pia itaendelea
kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri hiyo kupata haki ya kuamua hatma
yao.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment