Zaidi
ya wapalestina 25 wamejeruhiwa na jeshi la Israel katika kambi ya
Fawwar Ukingo wa Magharibi baada ya kuendesha operesheni Jumatatu
asubuhi katika maeneo tofauti.
Watu zaidi ya 25 wamejeruhiwa katika
mapambano ambayo yalitokea katika kambi ya wakimbizi Fawwar baina ya
jeshi la Israel na wapalestina. Kambi hiyo inapatika kwenye umbali
kidogo na Al Khalil kusini mwa Ukingo wa Magharibi kama washahidi wa
tukio walivyo fahamisha.
Kikosi cha jeshi la Israel kiliendesha
operesheni Jumatatu asubuhi katika kambi hiyo na kudai kuwa kilikuwa
kinataka kumtianguvuni mtu ambae alikuwa anatafutwa na mamlaka ya Israel
na baadae kuzua ghasia.
Katika ghasia hiyo vijana wakipalestina
waliwarushia wanajeshi wa Israel machupa huku jeshi likifyatua risasi
na mabomu ya kutoa machozi.
Home
Kimataifa
Slider
Zaidi ya wapalestina 25 wamejeruhiwa na jeshi la Israel katika kambi ya Fawwar Ukingo wa Magharibi
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment