Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni jijini Dar es
Salaam linawashikilia watuhumiwa watano akiwemo askari mgambo mmoja na
wanajeshi wanne kwa tuhuma za kuhusika
na mauaji ya mwendesha bodaboda aliyeuawa maeneo ya Mbezi Beach na Kutupwa
kando yam to.
![]() |
| ACP Charles Kenyela -Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondon |
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni ACP
Charles Kenyela, amesema kuwa watuhumiwa hao ambao majina yao yamehifadhiwa
watafikishwa mahakamani muda wowote kwa tuhuma za mauaji.
Amesema jeshi hilo linawashikilia watu 12 kwa tuhuma za
kufanya fujo, kujeruhi askari watatu kwa mawe, kuharibu mali pamoja na
kushambulia kituo cha Polisi cha kawe kwa madai ya kutaka kuwatoa watuhumiwa
waliokuwa wanadaiwa kumuua dereva wa boda boda.


0 comments:
Post a Comment