Viongozi
wa nchi na mashirka mbalimbali ya kimataifa yametoa salamu za rambirambi
kufuatia kifo cha waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Margaret Thatcher mwenye
umri wa miaka 87, ambaye alifariki jana asubuhi kutokana na ugonjwa wa kiharusi.
![]() |
| Margaret Thatcher - waziri mkuu wa zamani wa Uingereza. |
Waziri
mkuu wa Uingeraza David Cameron amesema, bibi Thatcher atakumbukwa kutokana na
umahiri wake katika siasa na ameifanya Uingereza isimame tena.
Hivyo
raia wa Uingereza hawana budi kumheshimu na kumshukuru.
Waziri
mkuu wa China Bw. Li Keqiang ametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha
Thatcher.
Katika
salamu zake za rambirambi, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amesema,
bi Thatcher ni mfano wa kuigwa na wanawake wengine duniani.
Serikali ya Uingereza inasema,
mazishi ya bi Thatcher yatafanya tarehe 17 Aprili katika kanisa ya St Paul's.
Serikali hiyo imeongeza kuwa, mazishi ya Bi Thatcher yatapewa hadhi sawa na
mama wa malkia Elizabeth II na Princess Dianna.


0 comments:
Post a Comment