Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU imeuagiza Uongozi wa Chuo kinachojiita 'Tanzania International University (TIU)' kilichopo Kimara Matangini jijini Dar es salaam kukifunga mara moja Chuo hicho ikiwemo kusitisha haraka zoezi la udahili wa wanafunzi pamoja na mchakato mzima wa uanzishwaji wa chuo hicho kutokana na kufanya shughuli zake kinyume cha sheria zilizowekwa na TCU.
 |
Prof. Magishi Nkwabi Mgasa - Katibu Mtendaji (TCU) Hayo yamebainishwa leo hii na Katibu Mtendaji (TCU) Prof. Magishi Nkwabi Mgasa wakati wa mazungumzo yake na Waandishi wa habari jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa (TCU) haijatoa Ithibati kwa chuo hicho inayokiruhusu kudahili wanafunzi ambapo kimekuwa kikijitangaza kuwa kinatoa kozi ngazi ya vyeti, stashahada na shahada na kuwataka wananchi kuwa makini na vyuo vya namna hiyo vinapojitokeza ili kuepuka usumbufu. |
 |
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo Aidha licha ya kukifunga chuo hicho, kimetakiwa kuondoa mabango yote yanayokitangaza chuo hicho, pamoja na kurudisha gharama zote ambazo zimekwishatolewa na wanafunzi hao walioanza zoezi la udahili, Sambamba na kuomba radhi kwa umma wa Watanzania na wadahiliwa kwa kuwadanganya kupitia vyombo vya habari. |
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment