Image
Image

EXCLUSIVE: BARAZA LA HABARITANZANIA MCT KUFANYA MKUTANO NA WAHARIRI MNJINI TANGA.

Baraza la Habari Tanzania (MCT) litafanya Mkutano wake wa pili wa mwaka  wa Mashauriano na Wahariri  mjini Tanga kuanzia Mei 29 hadi 30 mwaka huu.

Mkutano huo utafunguliwa na Waziri wa Sheria na Katiba , Bw. Mathias Chikawe.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema huu utakuwa ni mkutano wa pili  kufanyika hapa nchini, ambapo wahariri wapatao 50 kutoka  nchini kote watahudhuria. 
KAJUBI MUKAJANGA - KATIBU MTENDAJI MCT
Mkutano huo umeandaliwa mahsusi kuiwezesha MCT na Wahariri ambao ni watendaji muhimu katika vyombo vya habari, kukutana  na kujadiliana kuhusu masuala muhimu yanayohusiana na taaluma yao pamoja na changamoto ambazo vyombo vya habari vinakabiliana nazo, na hivyo kuweza kuangalia njia ya kuzipatia ufumbuzi.

Aidha kauli mbiu ya mwaka huu inasema: ìMwelekeo wa Tasnia ya Habari Tanzania Katika Muktadha wa Kujisimamia Wenyewe.î

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment