Tanzania na
China zimesaini makubaliano ya ushirikiano ambayo yataiwezesha wizara ya
mambo ya ndani ya nchi ya Tanzania na wizara ya usalama wa raia ya China
kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo kukabiliana na matukio ya uhalifu
wa kimataifa
![]() |
| BAADHI YA WACHINA WAKIWA WAMEKAA HUKU WAKISIKILIZA KWA USTADI , HATUA GANI YA MAKUBALIANO YA UTIAJI SAINI KATI YA TANZANIA NA NCHI YAO. |
Kupitia makubalino hayo maeneo yaliyoainishwa ni pamoja na ugaidi, uharamia, biashara ya dawa za kulevya, biashara haramu ya binadamu, usafirishaji wa fedha na wahamiaji haramu.
Makubaliano hayo yamesainiwa jijini Dar es salaam ambapo serikali ya Tanzania iliwakilishwa na waziri wa mambo ya ndani Dk. Emmanuel Nchimbi wakati kwa upande wa China aliyesaini makubaliano hayo ni naibu waziri wa wizara ya usalama wa raia bw. Yang Huanning.
![]() |
| YANG HUANNING - NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA USALAMA NA RAIA ( KUSHOTO) DK. EMMANUEL NCHIMBI ( KULIA) WAZIRI WA MAMBO YA NDANI TANZANIA, WAKITILIANA SANAINI. |
Kabla ya
kusaini makubaliano hayo, mawaziri hao walijadili masuala mbalimbali ikiwemo
namna ya kuimarisha ushirikiano katika upande wa mafunzo, ubadil;ishanaji wa
taarifa muhimu na upatikanaji wa vitendea kazi.
![]() |
| HUU NI MKONO WA YANG HUANNING - NAIBU WAZIRI WA CHINA AKITIA SANI . |
![]() |
| HUU NI MKONO WA DK. EMANUEL NCHIMBI - WAZIRI WA MAMBO YA NDANI TANZANIA, WAKATI AKITILIANA SAINI YA MAKUBALIANO KATIKA KUBADILISHANA UZOEFU WA KAZI NK. |
Licha ya
kusainiwa kwa makubaliano hayo, serikali ya China pia imetoa msaada wa vifaa
vya mawasiliano kwa jeshi la polisi ambavyo ni pamoja na radio 150 za mkononi
na radio za mezani 160 vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 393.
![]() |
| VIFAA VYA MAWASILIANO VILIVYOTOLEWA NA WAKENYA |
Kwaupande
wake Kamishna mwandamizi wa jeshi la polisi kitengo cha TEHAMA, AMDAN OMAR
MAKAME amesema kuwa vifaa hivyo vitasaidia sana katika kupambana na
uhalifu, na akawahakikishia wachina kuwa kwa vifaa walivyotoa watavitumia
ipasavyo ili kupunguza vitendo vya uhalifu nchini.
![]() |
| AMDAN OMAR MAKAME - KAMISHNA MWANDAMIZI JESHI LA POLISI . |







0 comments:
Post a Comment