Image
Image

EXCLUSIVE: KAMBI YA UPINZANI BUNGENI YAISHAURI SERIKALI KUSITISHA UUZAJI WA ARDHI KWA WAWEKEZAJI.

Kambi ya Upinzani Bungeni imeishauri serikali kusitisha uuzaji wa aridhi kwa wawekezaji wa kigeni na kufanya tathimini ili kubaini aridhi iliyokwisha uzwa imeleta tija gani kwa taifa.


Ushauri huo umetolewa bungeni mjini Dodoma na msemaji mkuu wa kambi hiyo kwa wizara ya Aridhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Halima Mdee, wakati wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka 2013/2014.

Bi. Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, amesema kupitia utafiti uliofanywa katika wilaya 79, unaonyesha kuwa umiliki wa aridhi ni mkubwa kwa wageni kuliko raia, kitu ambacho si kizuri kwa ustawi wa jamii.
Halima Mdee - Kawe - Mbunge wa kawe

Nayo, Kamati ya bunge ya Aridhi, Maliasili na Mazingira kupitia kwa mjumbe wake mbunge wa Viti Maalum (CCM) Dk. Mary Mwanjelwa, imezishauri mamlaka zinazosimamia mipango miji, kuzingatia sheria, kabla ya kutoa vibali vya ujenzi.
Dk. Mary Mwanjelwa -  Viti Maalum (CCM)
 Aidha, Mtoa hoja, Waziri wa Aridhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka alichukua wasaa huo kuzisihi benki za biashara nchini kuanza kuitumia kampuni ya Tanzania Mortgage Refinancing, ili ziweze kutoza riba ndogo kwa ajili ya mikopo ya nyumba.
Profesa Anna Tibaijuka - Waziri wa Ardhi.
 Katika wizara hiyo kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 108.3 kimeombwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment