Akizungumza
jijini Dar es Salaam wakati wa maonyesho ya bidhaa za ndani zikiwemo samani za
kiasili na za kisasa kutokana na miti,
mbao na udongo zenye asili ya Misri, Makamu wa Rais Dr Mohamed Gharib Bilal
amesema ipo haja ya kupanua wigo wa kibiashara miongoni mwa nchi za kiafrika
ili kuongeza ajira na ukuaji wa uchumi.
![]() |
| Dr Mohamed Gharib Bilal- Makamu wa rais Tanzania |
Amesema
serikali imechukua hatua mbalimbali zikiwemo za kuweka mazingira mazuri ya
uwekezeaji pamoja na kuondoa kero zilizokuwapo dhidi ya wawekezaji kutoka nje.
Hafla hiyo
ilihudhuriwa na mabalozi kutoka nchi mbali mbali hapa nchini.


0 comments:
Post a Comment