Hayo yamesemwa
na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mfuko wa taifa wa bima ya afya Balozi
Ali Mchumo wakati anafungua mkutano wa baraza kuu la wafanyakazi wa mfuko huo,
ambapo amesema kunahaja ya nchi kuwa na chombo kimoja kitakachosimamia
uendeshaji wa bima ya afya ili kuwezesha huduma inayotolewa kuwa na ubora
unaotakiwa na hata thamani ya fedha inayochangiwa na mwanachama ilingane na
huduma anayopata.
Aidha Balozi
Mchumo amesema changamoto inayoikabili NHIF ni kuendelea kutoa elimu ya umuhimu
wa wananchi kujiunga na mfuko wa taifa wa bima ya afya ili waweze kuwa na
uhakika wa afya zao.
![]() |
BALOZI ALI MCHUMO- MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI- NHIF.
|
Balozi
mchumo pia amesema malengo ya serikali ni ifikapo mwaka 2015 asilimia 30 ya
watanzania wawe wamefikiwa na huduma ya bima ya afya na mwaka 2025 watanzania
asilimia 75 wawe wamefikiwa na huduma hiyo,malengo aliyosema watayafikia iwapo
changamoto ya uhaba wa dawa kwenye maeneo ya kutolea huduma pamoja na lugha
mbovu kwa wateja yatarekebishwa.
Kwa upande wake
mwenyekiti wa TUGHE tawi la bima ya afya Baraka Maduhu amesema changamoto
inayowakabili wafanyakazi wa mfuko huo ni kuona namna gani wanaboresha huduma
za wanachama wao pamoja na kuongeza idadi ya wanachama ili watanzania wengi
waweze kunufaika na huduma za mfuko huo.


0 comments:
Post a Comment