Awali Waziri
mkuu Mizengo Pinda alitembelea baadhi ya maeneo yaliyoathirika na matukio ya
ghasia zinazodaiwa kuhusishwa na suala la gesi mkoani Mtwara wiki iliyopita.
Katika ziara
yake hiyo aliyofuatana na Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mikindani,Wilman Ndile,
Mbunge wa Wilaya ya Mtwara mjini, Hasni Murji na kamati ya Ulinzi na usalama ya
mkoa huo,Waziri mkuu ametembelea na kushuhudia uharibifu katika eneo la sabasaba ndani ya uzio wenye ofisi nyingi
ikiwemo taasisi ya uhasibu TIA,na kujionea namna ofisi ya ccm Chikongola
ilivyochomwa moto.
Aidha,amejionea
namna mahakama ya mwanzo ya Mikindani ilivyoharibiwa kufuatia ghasia hizo
ambapo imefahamishwa kwamba nyaraka nyingi zenye mahusiano na mashauri yaliyoko
mahakamani zilichomwa.
![]() |
|
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipewa
maelezo na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Wilman Ndile (kushoto) alipokwenda kuangalia
jengo la Mahakama ya Mwanzo Mitengo mjini Mtwara jana.
|
Amefika pia
katika ofisi ya mbunge,Hasni Murji iliyochomwa pia ambapo nyuma yake ilichomwa
baa ya mjasiriamali mmoja na ofisi ya
ccm kata Mtonya Mikindani na kusababisha hasara ya shilingi milioni 32.
Ameshuhudia
pia nyumba ya waziri wa TAMISEMI Ofisi ya Waziri Mkuu,Hawa Ghasia iliyochomwa
katika ghasia za mwezi Januari.
Kwa mjibu wa
maelezo aliyopewa waziri mkuu,uchomaji katika eneo hilo,ulifanyika kuanzia
majira ya saa nane mchana na vijana wenye umri wa miaka kati ya 16 na 25 huku
wakiwa wameficha nyuso zao.


0 comments:
Post a Comment