Image
Image

EXCLUSIVE: SERIKALI YASEMA UELEWA KWA WATANZANIA DHIDI YA UMUHIMU WA AFYA YAONGEZEKA

Na.Faraja Kihongole, Dar es Salaam.

Serikali imesema uelewa wa watanzania juu ya umuhimu wa bima ya afya kwa afya zao umeongezeka kufuatia maombi ya taasisi, makampuni na watu binafsi ya kutaka kujiunga na mfuko huo kuongezeka kwa kasi.

Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Mwinyi ameyasema hayo wakati anazindua bodi mpya ya tatu ya mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF, ambapo amesema pamoja na mwamko wa wananchi kutaka kujiunga na mfuko huo kuwa mkubwa tafiti za taifa za sekta ya afya zinaonyesha kuwa asilimia 40% ya gharama ya sekta ya afya ni fedha zinazotoka kwa wafadhili, asilimia 32% ni fedha kutoka kwenye mifuko ya wananchi, asilimia 26 fedha za serikali na asilimi mbili iliyobaki ndio zinatokana na bima mbalimbali za afya, hivyo bado kunachangamoto kubwa ya kuwafikia watanzania walio wengi.
Dk. Hussein Mwinyi - Waziri wa Afya Tanzania
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya Bw. Emmanuel Humba amesema pamoja na mafanikio yaliyopatikana kwenye mfuko huo, changamoto iliyopo mbele yao ni namna wanavyoweza kuboresha mfuko wa afya ya jamii CHF ambayo serikali imewapa dhamana ya kuuendesha huku mwenyekiti mpya wa bodi hiyo Balozi Ally Mchumo akisema moja ya kazi kubwa ya bodi yake ni kuhakikisha watanzania walio wengi wanajiunga na mfuko huo pamoja na kuimarisha huduma za matibabu kwa wanachama.

Uzinduzi wa bodi hiyo mpya ya NHIF ambayo inawajumbe tisa na itatumikia mfuko huo kwa muda wa miaka mitatu, ilihudhuriwa na wakurugenzi wote wa mfuko huo pamoja na mameneja wa mfuko kutoka mikoa yote ya bara na visiwani.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment