Msisitizo huo umetolewa na Mbunge wa Kuteuliwa na Rais Bw. James Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha (NCCR – MAGEUZI), na kuongeza kuwa maamuzi yaliyofanywa na baraza la mitihani la taifa (NECTA) yalikuwa na msukumo nyuma yake.
![]() |
| James Mbatia - Mbunge wa Kuteuliwa |
![]() |
| Shukuru Kawambwa - Waziri wa Elimu Tanzania |
Bw. Mbatia ambaye aliibuka bungeni na hoja binafsi ya kutokuwepo kwa mitaala rasmi katika elimu ya Tanzania, na hoja yake kupingwa, amesisitiza kuwa kulikuwa hakuna sababu kwa serikali kuunda tume ya kuchunguza kufeli kwa wanafunzi wa kidato cha nne, kwani mambo hayo yalikuwa ni ya kiutendaji na yalikuwa wazi.
Kutokana na serikali kukiri kuwa lipo tatizo katika sekta ya elimu, Mbunge huyo wa kuteuliwa amewataka wabunge wenzake, kubadilika na kuweka maslahi ya taifa mbele badala ya kuwa na itikadi za vyama, huku taifa likiendelea kuangamia.
| Wabunge wa Bunge la Tanzania - Wakiwa Bungeni Dodoma |



0 comments:
Post a Comment