Ofisi ya
Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema jumuiya ya kimataifa inashindwa
kutimiza wajibu wake kwa wahanga wa mzozo waSyriakwa kuruhusu vitendo vya
ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo kuendelea bila wahusika kuchukuliwa
hatua za kisheria.
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu Navi Pillay amesema hayo
wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Haki za Binadamu mjini Geneva, Uswisi
siku ya Jumatatu na kusema kuwa ukiukwaji huo wa haki za binadamu ni sawa na
uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu ambao hauwezi kuachiwa kuendelea
bila hatua kuchukuliwa.
![]() |
|
NAVI PILLAY - KAMISHNA MKUU WA HAKI ZA BINADAMU WA UM
|
Bi. Pillay amesema vikosi pinzani na serikali vinatumia
raia kama ngaoyao katika mapigano ilhali serikali yaSyria inaendelea kutumia
nguvu kupita kiasi na kushambulia bila kuchagua hata kwenye makazi ya raia,
pamoja na shule na hata hospitali.
Amesema umwagaji damu na mateso yanyokumba
wananchi waSyria yamekuwa hayavumiliki mbele ya binadamu.


0 comments:
Post a Comment