Image
Image

WADAU WA MICHEZO MKOANI TABORA WAKUMBUSHWA UMUHIMU WA KUWASAIDIA VIJANA.

Na. Juma Kapipi, kutoka Mkoani  Tabora.

Wadau  wa  soka  mkoani  Tabora  wamekumbushwa  umuhimu  wa  kuwasaidia  vijana  katika  michezo  ili  kutekeleza  dhana  nzima  ya  michezo  ni  ajira hatua  ambayo  pia  itawawezesha  kupunguza  kero  ya  ukosefu  wa  ajira kupitia  sekta  muhimu.

Akizungumza   mara  baada  ya  kukabidhi   vifaa  vya  michezo  kwa  mstahiki  Meya  wa  manispaa  ya  Tabora  kwa  ajili  ya  Jumuiya  ya  umoja  wa  vijana  wa  CCM  kata  ya  Kiloleni,mjumbe  wa  kamati  ya  uchumi   na  fedha   jumuiya  ya  Wazazi  mkoani  Tabora  ambaye  pia  ni  mlezi  vijana  Chipukizi,Emmanuel  Mwakasaka  ametoa  rai  hiyo  huku  akiwataka  vijana  kutopuuza  michezo  na  kuifanya  kuwa  ni  suluhisho  la  ukosefu  wa  ajira.

PICHA NA MAKTABA YETU.
 Aidha  Mwakasaka  pamoja  na  kuzungumzia  masuala  hayo  ya  michezo  alitumia  fursa  hiyo pia  kuwaasa  vijana  kutojihusisha  na  vitendo  vinavyoweza  kuathiri  maisha  yao  huku  wakiwa  bado  taifa  linawategemea  katika  masuala  mbalimbali  ya  kiuchumi.



PICHA NA MAKTABA YETU.
Kwa  upande wake  mstahiki  Meya  wa manispaa  ya  Tabora  Ghulam  Dewij  amempongeza  kada  huyo  wa  CCM  huku  akiwataka  wadau  wengine  wa  maendeleo  ya  michezo  mkoani  Tabora  kujitokeza  kwa  wingi  kuiga  mfano  huo  kwa  kusaidia  michezo  ya  aina  mbalimbali na  si kushia  katika  soka  pekee.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment