Image
Image

EXCLUSIVE: MWANAFUNZI UDOM AFARIKI BAADA YA KUJILIPUA NA PETROL NA KUJERUHI WANNE KWA WIVU WA MAPENZI



Kuringe Mongi, Dodoma

Mwanafunzi wa chuo cha ufundi stadi (VETA) Dodoma, Taliki Juma, amedaiwa kujilipua na moto wa petrol na kusababisha watu wanane kujeruhiwa na yeye mwenyewe kupoteza maisha, kutokana na kinachodaiwa kuwa wivu wa mapenzi.

Akizungumza na vyombo vya habari mjini Dodoma, Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Polisi Suzan Kaganda, amesema marehemu ambaye ni mwanafunzi wa fani ya magari, alisababisha mlipuko huo kwenye salon ya kutengenezea nywele, maeneo ya Nzuguni mjini Dodoma.

Chuo Cha UDOM
Inadaiwa kuwa siku ya tukio majira ya saa kumi jioni, marehemu Taliki ambaye ana umri wa miaka 22, aliingia kwenye salon ya Irene John Mapunda akiwa na galoni ya lita tano za petrol, ambapo alijimwagia mwilini pamoja na chumba alichokuwepo, na hatimaye kuwasha moto, uliosababisha mlipuko mkubwa.

Hata hivyo mmoja wa majeruhi wa mkasa huo Shaban Pili mwanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya sekondari ya City ya mjini Dodoma amelazwa kwenye hospitali ya mkoa wa dodoma.

Aidha majeruhi wote wa tukio hilo wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma na mwili wa marehemu Taliki, upo katika chumba cha maiti cha hospitali hiyo, ukisubiri taratibu za mazishi kutoka kwa ndugu zake.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment