Image
Image

Mpango wa usajili wa Sunderland kumchukua Jozy Altidore wakubaliwa na klabu yake ya AZ Alkmaar



Mshambuliaji wa AZ Alkmaar Jozy Altidore anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Sunderland baada ya vilabu hivyo viwili kukubaliana juu ya mpango wa mauzo ya nyota huyo raia wa Marekani.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ambaye amewahi kuichezea Hull City katika ligi kuu ya Englanda Premier League msimu wa 2009-10, anatarajiwa kuelekea England kwa ajili ya vipimo vya afya jumatatu.

Altidore alipokuwa na umri wa miaka 19 alijiunga na Hull City kwa mkopo wa muda mrefu akitokea Villarreal mwezi August 2009.


Alifunga goli zuri katika wa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Manchester City February 6 2010, likiwa ni goli lake pekee alilowahi kufunga katika jumla ya michezo 28 ya michezo ya ligi kuu ya England Premier League.

Alkmaar imethibitisha kuwepo kwa makubaliano kupitia mtandao wa klabu hiyo lakini imeshindwa kuweka wazi ni mpango wa kiasi gani cha fedha.

Altidore amesaliwa na miaka ndani ya mkataba wake na klabu hiyo ya kidachi.

Sunderland iliyochini ya Paolo Di Canio ikiwa itafanikiwa kumsajili  Altidore, itakuwa ni klabu ambayo ilikuwa bize kweli kweli katika zoezi la usajili kwani tayari imekuwa katika mipango ya kusajili wengine saba.

Sunderland kwa jina la utani Paka mweusi pia wamethibitisha kuwasajili akina Modibo Diakite, Valentin Roberge, Cabral, Duncan Watmore, David Moberg Karlsson na mlinda mlango Vito Mannone.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment