Image
Image

AFRIKA KUSINI YATAKA MGOGORO WA SYRIA UTATULIWE NA UN.



Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ndio chombo pekee kinachopaswa kufuatilia mgogoro wa Syria. 

Akizungumzia mabadiliko yanayojiri Syria, Zuma amesema, katika mkutano wa kundi la G20 uliofanyika huko Petersburg nchini Russia nchi nyingi hasa wanachama wa kundi la Bricks zilipinga mpango wa kushambuliwa Syria. 

Zuma aidha ameongeza kuwa, Umoja wa Mataifa ndio mahali bora zaidi pa kutatulia mgogoro wa Syria na masuala mengine yanayohusu usalama wa dunia.

Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi duniani zilizopinga waziwazi hatua ya Marekani ya kutaka kuishambulia kijeshi Syria.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment