Image
Image

UBALOZI MDOGO WA US AFGHANISTAN WASHAMBULIWA.



Watu wasiopungua watatu wameuawa na wengine 17 kujeruhiwa baada ya bomu la kutegwa garini kuripuka karibu na ubalozi mdogo wa Marekani huko Herat Afghanistan.

Sayed Fazlullah Wahidi, Gavana wa jimbo la Herat amesema shambulio hilo limetokea asubuhi ya leo ambapo bomu la kutegwa garini lililipuliwa umbali wa mita 60 kutoka ubalozi huo. 

Sauti ya mlipuko ilifuatiwa na milio ya risasi ambapo askari polisi wawili na afisa usalama wa ubalozi huo wameuawa huku watu wengine 17 wakijeruhiwa.  

Msemaji wa kundi la Taliban Qari Yousef Ahmadi ametangaza kuwa kundi hilo ndilo lililotekeleza shambulio hilo.

Shambulio hilo limejiri ikiwa ni siku mbili tangu wapiganaji wa Taliban wavurumishe makombora kadhaa katika kituo cha jeshi la anga cha Bagram ambacho ni kituo kikubwa zaidi cha kijeshi cha Marekani nchini Afghanistan.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment