Image
Image

MTANGAZAJI WA ITV UFOO SARO AHAMISHIWA MUHIMBILI BAADA YA TUMBI ALIKO KUWAKO MWANZO, YAELEZWA AMEJERUHIWA KWA RISASI MBILI SEHEMU YA TUMBO NA BEGA.



Mtangazaji wa Kituo cha Televiisheni cha ITV na redio one, Ufoo Saro, amejeruhiwa vibaya kwa risasi na mtu anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake baada ya kutokea kutoelewana baina yao majira ya asubuhi leo katika eneo la Kibamba wilaya ya kinondoni jijini Dar es salaam.

Kwa sasa ufoo Saro amehamishiwa kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili akitokea hospitali ya Tumbi,  na taarifa za awali inadaiwa amejeruhiwa kwa risasi kwenye bega na tumboni.

Taaarifa ambazo hazijathibitishwa inasemekana kulikua na ugomvi kati ya Ufoo na Mpenzi wake na baada ya kushindwa kuelewana waliamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo kwa ajili ya usuluhishi. 

Inadaiwa kuwa mwanaume huyo alimshutumu mama mkwe kwamba anamtetea mwanae na ndipo alipotoa bastola na kumpiga mama yake Ufoo Risasi ya kichwa na kumuua papo hapo, na kisha akampiga Ufoo Saro risasi mbili moja ya tumboni na nyingine ya begani akidhani amemuua kumbe amemjeruhi tu kisha akajipiga mwenyewe risasi ya kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.

Jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi kujua chanzo cha tukio hilo na limehaidi kutoa taarifa kamili wakati wowote.
Miili ya Marehemu mama yake Ufoo Saro pamoja na mpenzi wake Ufoo saro imehifadhiwa kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment