Image
Image

VIJANA ZAIDI YA 400 NCHINI TANZANIA KUSHIRIKI KONGAMANO LA KUMBU KUMBU YA MWALIMU NYERERE.



                         Mwl Julius Kambarege.

Na. AUGUSTINE MGENDI, BUTIAMA.
Zaidi ya Vijana 400 kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini wanatarajiwa kushiriki katika Kongamano la kuadhimisha Miaka 14 tangu kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarege Nyerere katika wilaya ya Butiama Mkoani Mara.

Kongamano hilo litakalofanyika Oktoba 14 katika eneo la Mwitongo wilaya ya Butiama mkoani Mara likiwa  limeandaliwa na Umoja wa Vijana Mkoa wa Mara,ofisi ya wilaya hiyo na Makumbusho ya hayati baba wa Taifa ambapo litakuwa na mada kuu mbili.

Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi Angelina Mabula amesema kuwa lengo la kongamano hilo kuwakumbusha Vijana juu ya falsafa za hayati baba wa Taifa ambapo Mkurugenzi mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku na Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrod Mkono watatoa Mada kuhusu Maendeleo vijijini na ajira kwa Vijana pamoja na miiko ya Viongozi.
                                  Angelina Mabula
Aidha baadhi ya Wazee wa eneo hilo la Butiama Mkoani hapa wameelezea mambo mbalimbali ambayo yameonekana miaka kumi na nne tangu kifo cha hayati baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Kongamano hilo litakuwa la Kwanza kufanyika wilayani hapa likiwa linahusisha Vijana Mbalimbali kutoka Tanzania katika kukumbushwa falsafa za hayati Mwalimu Julius Kambarege Nyerere ambapo Mkuu wa wilaya hiyo amesema litakuwa likifanyika kila Mwaka.");
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment