Image
Image

Miili ya wachimbaji wa mgodi wa dhahabu waliokuwa wamefukiwa na kifusi ya opolewa Geita



Hatimaye wachimbaji wote watatu waliokufa kwa kufukiwa na kifusi cha jabali katika mgodi wa dhahabu wa Onesmo Goldmine Mawemeru uliopo katika kijiji cha Nyalugusu Wilayani Geita imeopolewa jana usiku baada ya juhudi za siku nne.

Hatua hiyo imedaiwa ni matokeo ya ushirikiano na mshikamano mkubwa uliooneshwa katika kutekeleza zoezi hilo kati ya Uongozi wa Mgodi huo, wadau na serikali ya wilaya na mkoa zoezi lililokuwa linafanyika usiku na mchana kwa kushirikisha wadau tofauti na hivyo kufanikiwa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Joseph Konyo akithibitisha LEO kupatikana kwa miili hiyo alisema kazi hiyo ilihitaji ujasiri na kujituma na ndicho kilichofanyika kuhakikisha miili yote mitatu imeopolewa.Bofya kusoma habari hii kwa kina->http://www.eatv.tv/news/current-affairs/miili-ya-waliofukiwa-kifusi-mgodini-yaopolewa

Amewataja miili yao walioopolewa kuwa ni Benjamin Yusuph, Robert Edward na Nsulwa Bungila ambao wote walifukiwa katika mgodi huo Januari 11 saa moja usiku na wengine wanne Samson Haroun, Rutu William, Faida Bukombe na Seif Ally waliokolewa siku ya tukio.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment