Image
Image

Vyanzo vya maji zaidi ya 40 vya kauka kutokana na uharibifu wa mazingira Mbeya.

Kasi ya uharibifu wa misitu ya hifadhi ya safu za mlima mbeya imesababisha zaidi ya vyanzo vya maji 40 kukauka katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, hali ambayo imeushtua uongozi wa mkoa wa mbeya ambao sasa umebuni mpango wa kuhifadhi mistitu hiyo kwa kuwashirikisha wadau wote wa mazingira koani mbeya.

Akizindua mpango huo wa kuhifadhi misitu ya safu za mlima mbeya na kuongoza zoezi la upandaji wa miti zaidi ya 200 katika kata ya iziwa, mkuu wa mkoa wa mbeya abbas kandoro amesema mkoa wa mbeya una jumla ya misitu 142 ambayo inahifadhiwa, lakini kati yake misitu 20 ni muhimu zaidi kutokana na kuwa ipo kwenye vyanzo vya maji vinavyotegemewa na wakazi wote wa mkoa wa mbeya, hivyo akawataka wananchi wote kushiriki kuilinda.

Kwa upande wake, afisa mazingira wa baraza la taifa la mazingira (NEMC), kanda ya nyanda za juu kusini, nzwamkulu ezekiel amesema kuwa lengo la mpango huo ni kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji vya eneo hilo, huku mwakilishi wa bodi ya bonde la maji la ziwa rukwa, mkwanjilwa watson akitoa wito kwa wananchi kutumia maji kiuchumi ili waweze kujiletea maendeleo.

Baadhi ya wadau wa mazingira mkoani mbeya wamesema kuwa mpano huo ukitekelezwa kama ulivyopangwa unaweza kurejesha uoto wa asili ambao umeanza kutoweka katika safu za milima hiyo na maeneo mengine.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment