Image
Image

Mwanamke auawa kutokana na wivu wa kimapenzi Sinyanga



Mkazi  wa mtaa wa Kitwana kata ya Busoka wilayani Kahama mkoani Shinyanga Regina  Shija (55) ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga kichwani  na watu wasiojulikana kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa Kimapenzi.

Afisa mtendaji wa Mataa huo, Bw. Rafael Jumanne ameiambia ITV kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 5.00 usiku ambao watu wasiofahamika walivamia nyumbani kwa  Regina akiwa  anajiandaa kulala na wajukuu wake wawili. 
Amesema baada ya watu hao ambao idadi yao haijafahamika, kuvamia nyumbani hapo walianza kumkatakata mapanga mama huyo kichwani na  mkono wa kulia hali iliyosababisha kuvuja damu kwa wingi baadaye kufariki dunia.

Afisa Mtendaji huyo amedai kuwa chanzo cha  mauji hayo bado hakijafahamika ingawa yanahusishwa na wivu  wa kimapenzi na kwamba   jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu huyo na kuupeleka kuuhifadhi katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya wilaya ya Kahama.Kwa taarifa zaidi Bofya hapahttp://www.itv.co.tz/news/local/1588-16591/Mwanamke_auawa_kwa_kukatwakatwa_mapanga_kwa_kile_kinachodaiwa_wivu_wa_mapenzi.html
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment