Image
Image

Membe aelekea Urus kwa ziara ya kikazi ya siku Tatu


                              TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) ameondoka nchini tarehe 13 Januari 2015 kwenda Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Mhe. Sergey Lavrov. Ziara hiyo inalenga kuimarisha na kupanua ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi.

Mhe. Membe anatarajiwa kutumiafursa hiyo kuhimiza ushirikiano wa kiuchumi na Urusi, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji na ubadilishanaji wa teknolojia.  Tanzania inaweza kufaidika na utaalamu wa Urusi katika sekta za uzalishaji wa nishati, uvuvi, afya, kilimo na huduma. 
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Tarehe 14 Januari, 2015.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment